-
Uadilifu Si kwa Mapokeo ya MdomoMnara wa Mlinzi—1990 | Oktoba 1
-
-
12. (a) Yesu alifanya badiliko gani la kuiacha njia yake ya kawaida ya kutoa utangulizi wenye kurejezea Maandiko ya Kiebrania katika Mahubiri yake juu ya Mlima, na kwa nini? (b) Twajifunza nini kutokana na utumizi wa sita wa usemi “Imesemwa”?
12 Yesu aliponukuu kutokana na Maandiko ya Kiebrania hapo kwanza, alisema hivi: “Imeandikwa.” (Mathayo 4:4, 7, 10) Lakini mara sita katika yale Mahubiri juu ya Mlima, alifanya utangulizi wa zile zilizosikika kama taarifa za kutoka kwenye Maandiko ya Kiebrania kwa maneno haya: “Ilisemwa.” (Mathayo 5:21, 27, 31, 33, 38, 43, NW) Kwa nini? Kwa sababu alikuwa akirejezea Maandiko kama yalivyofasiriwa kulingana na mapokeo ya Kifarisayo yaliyopinganisha amri za Mungu. (Kumbukumbu 4:2; Mathayo 15:3) Hilo laonyeshwa wazi katika rejezo la Yesu la sita lililo la mwisho katika mfululizo huu: “Mmesikia [mlisikia, NW] kwamba imenenwa [ilisemwa, NW], Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako.” Lakini hakuna sheria yoyote ya Kimusa iliyosema, “Umchukie adui yako.” Waandishi na Mafarisayo ndio waliosema hivyo. Hiyo ilikuwa ndiyo fasiri yao ya Sheria ya kupenda jirani yako—jirani yako Myahudi, hakuna wengine.
-
-
Uadilifu Si kwa Mapokeo ya MdomoMnara wa Mlinzi—1990 | Oktoba 1
-
-
17. Yesu alifundisha kufuata njia gani bora kuliko “jicho kwa jicho, na jino kwa jino”?
17 Ndipo Yesu akasema: “Mmesikia kwamba imenenwa, Jicho kwa jicho, na jino kwa jino; lakini mimi nawaambia, Msishindane na mtu mwovu; lakini mtu akupigaye shavu la kuume, mgeuzie na la pili.” (Mathayo 5:38-42) Hapa Yesu harejezei pigo lenye madhumuni ya kuumiza bali kofi la madharau kwa kutumia upande wa nyuma wa mkono. Wewe mwenyewe usijishushie hadhi kwa kurudisha madharau. Kataa kurudisha ovu kwa ovu. Bali, rudisha wema na hivyo “uushinde ubaya kwa wema.”—Warumi 12:17-21.
-