-
Uadilifu Si kwa Mapokeo ya MdomoMnara wa Mlinzi—1990 | Oktoba 1
-
-
17. Yesu alifundisha kufuata njia gani bora kuliko “jicho kwa jicho, na jino kwa jino”?
17 Ndipo Yesu akasema: “Mmesikia kwamba imenenwa, Jicho kwa jicho, na jino kwa jino; lakini mimi nawaambia, Msishindane na mtu mwovu; lakini mtu akupigaye shavu la kuume, mgeuzie na la pili.” (Mathayo 5:38-42) Hapa Yesu harejezei pigo lenye madhumuni ya kuumiza bali kofi la madharau kwa kutumia upande wa nyuma wa mkono. Wewe mwenyewe usijishushie hadhi kwa kurudisha madharau. Kataa kurudisha ovu kwa ovu. Bali, rudisha wema na hivyo “uushinde ubaya kwa wema.”—Warumi 12:17-21.
-
-
Uadilifu Si kwa Mapokeo ya MdomoMnara wa Mlinzi—1990 | Oktoba 1
-
-
20. Badala ya kuiweka kando Sheria ya Kimusa, Yesu aliongezeaje upana na kina cha uzito wayo na kuiweka kwenye kiwango cha juu hata zaidi?
20 Hivyo basi Yesu aliporejezea sehemu za Sheria na kuongezea, “Lakini mimi nawaambia,” hakuwa akiiweka kando Sheria ya Kimusa na kuweka kitu kingine mahali payo. Sivyo, bali alikuwa akiongeza kina na upana wa kani yayo kwa kuonyesha roho iliyokuwa kusudi la kuwako kwayo. Sheria ya juu zaidi ya udugu yahukumu uhasama wenye kuendelea kuwa ni uuaji. Sheria ya juu zaidi ya utakato yashutumu fikira ya kuendelea na nyege za tamaa mbaya kuwa uzinzi. Sheria ya juu zaidi ya ndoa yakataa kutaliki bila sababu ya maana kuwa ni mwendo unaoongoza kwenye kufunga upya ndoa za uzinzi. Sheria ya juu zaidi ya ukweli yaonyesha kuwa si lazima kuapa-apa. Sheria ya juu zaidi ya upole yaweka kando kulipa kisasi. Sheria ya juu zaidi ya upendo yataka upendo wa kimungu usio na mipaka.
-