-
Waroma 15:26, 27Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
26 Kwa maana wale wenye kuwa katika Makedonia na Akaya wamependezwa kushiriki vitu vyao kwa kuwatolea muchango fulani wale wenye kuwa maskini kati ya watakatifu katika Yerusalemu.+ 27 Kweli, wamependezwa kufanya vile, na kwa hakika walikuwa na deni kwao; kwa maana kama mataifa wameshiriki mambo yao ya kiroho, wao pia wako na deni la kuwatumikia kwa vitu vyao vya kimwili.+
-
-
Wafilipi 4:15-17Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
15 Kwa kweli, ninyi Wafilipi pia munajua kwamba kisha ninyi kujifunza habari njema pale mwanzo, wakati nilitoka Makedonia, hakuna kutaniko lenye lilishiriki pamoja na mimi katika kutoa na kupokea, isipokuwa ninyi tu;+ 16 kwa maana wakati nilikuwa Tesalonike, mulinitumia kitu kwa ajili ya mambo yenye nilikuwa nayo lazima, haikukuwa mara moja tu lakini mara mbili. 17 Haiko kusema ninatafuta zawadi, lakini ninataka matunda yenye kuleta faida zaidi kwenye akiba yenu.
-