Isaya
5 Tafadhali, acha nimwimbie mpenzi wangu wimbo wa mpenzi wangu kuhusu shamba lake la mizabibu.+ Palikuwa na shamba la mizabibu ambalo mpenzi wangu alikuwa nalo kando ya kilima chenye kuzaa sana. 2 Naye akalilima na kuliondoa mawe na kulipanda mzabibu bora mwekundu, na kujenga mnara katikati yake.+ Na pia kulikuwa na shinikizo la divai ambalo alichimba ndani yake.+ Naye akaendelea kulitumaini lizae zabibu,+ lakini mwishowe likazaa zabibu-mwitu.+
3 “Na sasa, enyi wakaaji wa Yerusalemu nanyi watu wa Yuda, tafadhali hukumuni kati yangu na shamba langu la mizabibu.+ 4 Kuna kitu gani ambacho bado sijalifanyia shamba langu la mizabibu, ambacho bado sijafanya ndani yake?+ Kwa nini nilitumaini lizae zabibu, lakini mwishowe likazaa zabibu-mwitu? 5 Na sasa, tafadhali, acheni niwajulishe ninyi kitu nitakacholifanyia shamba langu la mizabibu: Ukigo wake utaondolewa,+ nalo halitakosa kuteketezwa kwa moto.+ Ukuta wake wa mawe utabomolewa, nalo halitakosa kuwa mahali pa kukanyaga-kanyaga.+ 6 Nami nitaliweka kuwa kitu kilichoangamizwa.+ Nalo halitapunguzwa matawi, wala halitalimwa.+ Nalo litamea vichaka vya miiba na magugu;+ nami nitayaamuru mawingu yasinyeshe mvua yoyote juu yake.+ 7 Kwa maana shamba la mizabibu+ la Yehova wa majeshi ni nyumba ya Israeli, na watu wa Yuda ndilo shamba alilolipenda.+ Naye akaendelea kutumaini hukumu+ ifanywe, lakini, tazama! ikawa ni kuvunjwa kwa sheria; kutumaini uadilifu ufanywe, lakini, tazama! ikawa ni kilio.”+
8 Ole wao wanaounganisha nyumba na nyumba,+ na wale wanaounganisha shamba na shamba hata nafasi isiwepo tena+ nanyi mmefanywa mkae peke yenu kabisa katikati ya nchi! 9 Yehova wa majeshi ameapa masikioni mwangu kwamba nyumba nyingi, ingawa ni kubwa na nzuri, zitakuwa kitu cha kushangaza kabisa, bila mkaaji.+ 10 Kwa maana hata ekari kumi+ za shamba la mizabibu zitazaa kipimo kimoja tu cha bathi,+ na hata kipimo kimoja cha homeri ya mbegu kitazaa kipimo kimoja tu cha efa.+
11 Ole wao wanaoamka asubuhi na mapema ili watafute tu kileo,+ wanaokawia mpaka giza la jioni sana hivi kwamba divai inawawasha!+ 12 Na kutakuwa na kinubi na kinanda, tari na filimbi, na divai katika karamu zao;+ lakini hawauangalii utendaji wa Yehova, wala hawakuiona kazi ya mikono yake.+
13 Kwa hiyo watu wangu watalazimika kwenda uhamishoni kwa sababu ya kukosa ujuzi;+ na utukufu wao utakuwa ni watu wenye njaa,+ na umati wao utakaushwa kwa kiu.+ 14 Kwa hiyo Kaburi* limeipanua sana nafsi yake nalo limekipanua kinywa chake kwa kupita mipaka;+ na kilicho cha fahari ndani yake, pia umati wake na ghasia yake na mwenye kufurahi, hakika wataingia ndani yake.+ 15 Na mtu wa udongo atainama, na mwanadamu atashuka, na hata macho ya walio juu yatashuka.+ 16 Na Yehova wa majeshi atakuwa juu kupitia hukumu,+ na Mungu wa kweli, aliye Mtakatifu,+ hakika atajitakasa kupitia uadilifu.+ 17 Na wana-kondoo dume kwa kweli watalisha kana kwamba katika malisho yao; na mahali penye ukiwa pa wanyama waliolishwa vizuri pataliwa na wakaaji wageni.+
18 Ole wao wanaovuta kosa kwa kamba zisizosema kweli, na dhambi kana kwamba ni kwa kamba za gari la kukokotwa;+ 19 wale wanaosema: “Kazi yake na iharakishe; hiyo na ije upesi ili tuione; nalo shauri la Mtakatifu wa Israeli likaribie na kuja, ili tupate kulijua!”+
20 Ole wao wanaosema kwamba wema ni ubaya na ubaya ni wema,+ wale wanaoweka giza badala ya nuru na nuru badala ya giza, wale wanaoweka uchungu badala ya utamu na utamu badala ya uchungu!+
21 Ole wao walio na hekima machoni pao wenyewe, walio na busara mbele ya nyuso zao wenyewe!+
22 Ole wao walio na nguvu katika kunywa divai, na wanaume walio na nguvu za kuchanganya kileo,+ 23 wale wanaomtangaza mtu mwovu kuwa mwadilifu kwa kufikiria rushwa,+ na wanaomwondolea mwadilifu hata uadilifu wake!+
24 Kwa hiyo kama mwali wa moto unavyoteketeza majani makavu+ na kama majani matupu yanavyoingia ndani ya miali ya moto, ndivyo kisiki chao kitakavyokuwa kama harufu ya kuoza,+ na ua lao litaenda juu kama mavumbi, kwa sababu wameikataa sheria ya Yehova wa majeshi,+ nao wamelidharau neno la Mtakatifu wa Israeli.+ 25 Ndiyo sababu hasira ya Yehova imewaka juu ya watu wake, naye atanyoosha mkono wake juu yao na kuwapiga.+ Na milima itatetemeka,+ na maiti zao zitakuwa kama takataka katikati ya barabara.+
Kwa sababu ya hayo yote hasira yake haijarudi nyuma, bali mkono wake bado umenyooshwa. 26 Naye ameliinulia ishara taifa kubwa lililoko mbali,+ na amelipigia mluzi kwenye mwisho wa dunia;+ na, tazama! likiwa na haraka litaingia upesi.+ 27 Hakuna yeyote aliyechoka wala hakuna yeyote anayejikwaa katikati yao. Hakuna yeyote anayesinzia wala hakuna yeyote anayelala. Na mshipi ulio viunoni mwao hakika hautafunguliwa, wala kamba za viatu vyao hazitakatwa vipande viwili; 28 kwa sababu mishale yao imenolewa na pinde zao zote zimepindwa.+ Kwato za farasi wao zitahesabiwa kuwa jiwe,+ na magurudumu yao kama upepo wa dhoruba.+ 29 Kunguruma kwao ni kama kule kwa simba, nao hunguruma kama wana-simba wenye manyoya shingoni.+ Nao watanguruma na kuyakamata mawindo na kuyapeleka salama, wala hapatakuwa na mkombozi.+ 30 Nao siku hiyo watanguruma juu yake na mngurumo kama wa bahari.+ Na mtu kwa kweli ataiangalia nchi, na, tazama! kuna giza lenye kutaabisha;+ na hata nuru imetiwa giza kwa sababu ya matone yanayoanguka juu yake.