1 Wakorintho
4 Acheni mtu atukadirie sisi hivyo kuwa tuko chini ya+ Kristo nasi ni wasimamizi-nyumba+ wa siri takatifu+ za Mungu. 2 Mbali na hilo, katika hali hii, kinachoangaliwa katika wasimamizi-nyumba+ ni mtu kupatwa akiwa mwaminifu.+ 3 Basi kwangu ni jambo dogo sana kwamba ninyi au baraza la kibinadamu mnichunguze.+ Hata mimi sijichunguzi mwenyewe. 4 Kwa maana sifahamu+ kitu chochote dhidi yangu mwenyewe. Lakini kwa hilo sionyeshwi kuwa mwadilifu, bali yeye anayenichunguza ni Yehova.+ 5 Kwa hiyo msihukumu+ kitu chochote kabla ya wakati unaofaa, mpaka Bwana aje,+ atakayeyaleta kwenye nuru mambo ya siri yaliyo ya giza+ na pia kuyafunua mashauri ya mioyo,+ na ndipo kila mtu atakapopata sifa yake kutoka kwa Mungu.+
6 Basi, akina ndugu, mambo haya nimeyahamisha ili kuyatumia juu yangu mwenyewe na Apolo+ kwa faida yenu, ili katika hali yetu mjifunze kanuni: “Msipite mambo yaliyoandikwa,”+ ili msijivune+ mtu mmoja-mmoja kwa kumpendelea mtu mmoja juu ya mwingine.+ 7 Kwa maana ni nani anayekufanya wewe kuwa tofauti+ na mwingine? Kwa kweli, una nini ambacho hukupokea?+ Basi, ikiwa kwa kweli ulikipokea,+ kwa nini unajisifu+ kana kwamba hukukipokea?
8 Ninyi tayari mmepata shibe yenu, sivyo? Ninyi tayari ni matajiri, sivyo?+ Mmeanza kutawala mkiwa wafalme+ bila sisi, sivyo? Nami ningalipenda kwamba muwe mmeanza kutawala mkiwa wafalme, ili sisi pia tutawale pamoja nanyi tukiwa wafalme.+ 9 Kwa maana inaonekana kwangu kwamba Mungu ametuweka sisi mitume mwisho katika wonyesho wa hadharani+ kama watu waliowekewa kifo,+ kwa sababu tumekuwa tamasha+ kwa ulimwengu, na kwa malaika,+ na kwa wanadamu.+ 10 Sisi ni wapumbavu+ kwa sababu ya Kristo, lakini ninyi ni wenye busara+ katika Kristo; sisi ni dhaifu,+ lakini ninyi ni wenye nguvu;+ ninyi mna sifa njema,+ lakini sisi tumo katika aibu.+ 11 Mpaka saa hii sisi tunaendelea kupata njaa+ na pia kupata kiu+ na kuvaa mavazi machache+ na kupigwa+ huku na huku na kuwa bila makao+ 12 na kufanya kazi ya kutaabika,+ tukifanya kazi kwa mikono yetu wenyewe.+ Tunapotukanwa, tunabariki;+ tunapoteswa, tunavumilia;+ 13 tunapoharibiwa sifa, tunasihi;+ tumekuwa kama takataka ya ulimwengu, uchafu wa vitu vyote, mpaka sasa.+
14 Ninaandika mambo haya, si ili kuwaaibisha ninyi, bali kuwaonya kama watoto wangu wapendwa.+ 15 Kwa maana ingawa huenda mkawa na watunzaji+ elfu kumi katika Kristo, hakika hamna baba wengi;+ kwa maana katika Kristo Yesu mimi nimekuwa baba yenu kupitia habari njema.+ 16 Kwa hiyo, nawasihi ninyi, iweni waigaji wangu.+ 17 Ndiyo sababu ninamtuma Timotheo kwenu,+ kwa kuwa yeye ni mtoto wangu mpendwa+ na mwaminifu katika Bwana; naye atawakumbusha ninyi njia zangu kuhusiana na Kristo Yesu,+ kama vile ninavyofundisha kila mahali katika kila kutaniko.
18 Wengine wamejivuna+ kana kwamba siji kwenu. 19 Lakini nitakuja kwenu hivi karibuni, Yehova akipenda,+ nami nitajua, si maneno ya wale ambao wanajivuna, bali nguvu zao. 20 Kwa maana ufalme wa Mungu hauko katika maneno, bali katika nguvu.+ 21 Mnataka nini? Je, nije kwenu nikiwa na fimbo,+ au kwa upendo na upole wa roho?+