Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w90 12/1 kur. 3-5
  • Ni Mungu Yupi Ambaye Wewe Unaabudu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ni Mungu Yupi Ambaye Wewe Unaabudu?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Ibada Mchanganyiko
  • “Jilindeni Nafsi Zenu na Sanamu”
  • Kuabudu Pesa
  • Umwabudu Mungu Yupi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Ni Ibada ya Nani Anayoikubali Mungu?
    Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele
  • Je! Wewe Utakuwa Shahidi kwa Ajili ya Yule Mungu wa Kweli?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Kesi ya Mahakama ya Ulimwengu Wote Mzima Ambayo Inakuhusisha Wewe Ndani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
w90 12/1 kur. 3-5

Ni Mungu Yupi Ambaye Wewe Unaabudu?

KOTE ulimwenguni, watu wangejibu swali hilo kwa njia nyingi tofauti. Mtume Paulo alisema hivi: “Wako miungu na mabwana wengi,” na leo kuna mamilioni ya miungu yenye kuabudiwa. (1 Wakorintho 8:5, HNWW) Hata hivyo, je! ulijua kwamba watu wengi wanaabudu mungu tofauti na yule ambaye wao wanafikiri wanamwabudu? Na je! ulifahamu kwamba wengi wasioamini kuna Mungu wana bidii sana kuliko wale wenye kuamini mungu fulani? Kwa njia gani?

Basi, maana moja ya kuabudu ni “kuchukua kwa staha, heshima, au ujitoaji mkubwa, hata wa kupita kiasi.” Katika lugha za kwanza za Biblia, maneno ya ibada yana wazo la utumishi au kuinama mbele ya mtu fulani. Kwa kufikiria hilo, acheni tuone jinsi watu wanaweza kukosea wanaabudu nani au nini hasa.

Ibada Mchanganyiko

Chukua mfano wa Wasamaria wa kale. Hapo kwanza wengi wao walikuwa wageni walioingizwa na Waashuri katika Palestina ili wachukue mahali pa makabila kumi ya kaskazini ya Israeli yaliyohamishwa. Kabla ya hapo, walikuwa wamefuata miungu ya kipagani, lakini sasa walijitahidi kujifunza juu ya Yehova, Mungu wa Israeli. Je! ndipo waliacha dini yao ya zamani? Sivyo. Biblia inaripoti hivi: “Wakafanya sawasawa na kawaida zao za kwanza. Basi mataifa hawa wakamcha BWANA [Yehova, NW], tena wakaziabudu sanamu zao za kuchongwa.” (2 Wafalme 17:40, 41) Hivyo basi ingawa kwa kawaida Wasamaria walimtambua Yehova,  bado walitumikia miungu yao ya zamani, hivyo kuzoea aina ya dini mchanganyiko.

Jambo fulani kama hilo lilitendeka wakati wamisionari walipoingiza Ukatoliki wa Kiroma ndani ya Amerika ya Kusini. Waligeuza sehemu kubwa ya watu, lakini kama Wasamaria wa kale, watu hawakusahau miungu yao ya zamani. Hivyo, katika Brazili desturi za kipagani za uchawi zingali zinashikwa na “Wakristo,” hali moja na miadhimisho inayoheshimu miungu ya kale, kama mungu-mke Iemanjá. Mambo kama hayo yatukia katika nchi nyingine za Amerika ya Kusini.

Tena, dini ambayo wamisionari hao waliingiza katika Amerika ya Kusini ilikuwa dini mchanganyiko hiyo yenyewe. Mengi ya mafundisho yake, kama Utatu, moto wa mateso, na kutokufa kwa nafsi, yalitokana na dini na falsafa za kale za kipagani. Hakika hazikupatikana katika Biblia. Vivyo hivyo, sikukuu zayo—kutia na Krismasi na Ista—zilikuwa na mwanzo usio wa Kikristo.a Je! yawezekana kushika sikukuu hizo za kipagani na kuamini katika mafundisho hayo yasiyo ya Kikristo na bado kumwabudu Mungu wa Biblia, aliyesema hivi: “Usiwe na miungu mingine ila mimi”? (Kutoka 20:3) Hakika sivyo!

“Jilindeni Nafsi Zenu na Sanamu”

Fikiria njia nyingine ambayo watu wanadanganywa katika ibada. Mtume Yohana aliandika hivi: “Watoto wadogo, jilindeni nafsi zenu na sanamu.” (1 Yohana 5:21) Watu karibu milioni elfu moja wamepangwa katika orodha kuwa ni wa Jumuiya ya Wakristo, na inasemwa kwamba wao wanadai kumwabudu Mungu yule yule ambaye Yohana alimwabudu. Hata hivyo, mamia ya mamilioni kati yao wanainamia mifano ya “watakatifu,” ya Yesu, na ya bikira Mariamu.

Kuna namna nyingi zaidi za ibada ya sanamu zisizoonekana wazi. Katika mwaka 44 W.K., Mfalme Herode Agrippa alitoa hotuba ya watu wote, na watu wakasisimuka sana hata wakapaaza sauti hivi: “Ni sauti ya Mungu, si sauti ya mwanadamu”! (Matendo 12:21, 22) Ndiyo, walimwabudu Herode kuwa sanamu, wakimfanya mungu. Mambo kama hayo hutendeka leo. Katika zile siku zenye mafanikio makubwa ambapo Unazi ulikuwa ukiinuka kwenye mamlaka katika Ulaya, kilio “Heil Hitler!” kwa kweli kilikuwa mpaazo wa sauti ya ibada. Wengi walikuwa na nia ya kupigana na kufa kwa ajili ya Führer (Kiongozi) kana kwamba alikuwa mungu, mwokozi wa taifa. Hata hivyo, walio wengi wa wale wenye kutoa heshima kuu hiyo walikuwa washiriki wa makanisa ya Jumuiya ya Wakristo!

Kabla na baada ya Hitler, viongozi wengine wa kisiasa wamejikuza hivyo hivyo kuwa waokozi na kudai ujitoaji usiotia mwingine ndani. Wale waliojiachilia waliwafanya wanadamu hawa kuwa miungu, bila kujali “waabudu” hao walikuwa wa dini gani rasmi au hata kama walidai kuwa hawaamini kuna Mungu. Heshima kuu ambayo majogoo wenye vipawa vya michezo, majogoo wa sinema, na wafurahishi wengine hupokea kutoka kwa wanaowapenda sana ni kama ibada.

Kuabudu Pesa

Zaidi ya hilo, fikiria maana ya maneno ya Yesu aliposema hivi: “Hakuna mtu awezaye kutumikia mabwana wawili; kwa maana atamchukia huyu, na kumpenda huyu; ama atashikamana na huyu, na kumdharau huyu. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali.” (Mathayo 6:24) Je! wewe unajua mtu yeyote ambaye ni wa dini fulani lakini upendezi wake mkuu maishani ni kutafuta pesa? Basi, kwa kweli huyo anatumikia nani, Mungu au mali? Wewe unajua wasioamini wangapi ambao wamenaswa sana katika mfuatio wa pesa? Hakika, wao pia ni waabudu pesa, labda wakiwa na bidii kuliko waamini wengi.

Mtume Paulo alieleza kanuni kama hiyo alipoandika hivi: “Basi, vifisheni viungo vyenu vilivyo katika nchi, uasherati, uchafu, tamaa mbaya, mawazo mabaya, na kutamani, ndiyo ibada ya sanamu.” (Wakolosai 3:5) Tukitamani sana kitu fulani hivi kwamba twa-tumia jitihada zetu zote kuelekea kukipata, labda hata kuvunja sheria katika mwendo huo, hapo basi kitu hicho ni sanamu, ni mungu, kwetu. (Waefeso 5:5) Katika barua nyingine, Paulo aliandika hivi juu ya watenda kosa fulani: “Tumbo lao ndio mungu wao.” (Wafilipi 3:19, HNWW) Ikiwa kusudi letu zima maishani ni kujipendeza wenyewe, kama kujaza tumbo letu, basi sisi ndio mungu wetu wenyewe. Wewe unajua watu wangapi wanaoabudu mungu wa aina hii?

Ndiyo, kama mtume Paulo alivyoandika: “Wako miungu na mabwana wengi.” Na katika visa vingi, waabudu wao ni kama Wasamaria wa kale, wakitumikia mungu mmoja kwa maneno yao na mwingine kwa vitendo vyao. Ingawa hivyo, kwa kweli kuna Mungu mmoja tu astahiliye ibada yetu. Je! wewe unajua yeye ni nani? Zaidi ya hilo, kuna jambo moja ambalo linaunganisha ibada ya miungu mingine yote mbali na yeye. Nini hilo? Tutaona katika makala inayofuata.

[Maelezo ya Chini]

a Kwa habari zaidi, ona kitabu Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani, kurasa 212-13, kilichochapishwa na Watchtower Bible and Tract Society of New York.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki