Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Leo
Novemba
Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2018

Jumapili, Novemba 18

Mlipolipokea neno la Mungu, . . . mlilikubali . . . kama lilivyo kwa kweli, kama neno la Mungu.—1 The. 2:13.

Watumishi wa Yehova wanaiheshimu sana Biblia, kitabu kitakatifu cha Mungu. Kwa kuwa sisi si wakamilifu, tunahitaji mashauri mara kwa mara kutoka kwenye Maandiko. Tunatendaje tunaposhauriwa? Wafikirie Euodia na Sintike, Wakristo wa karne ya kwanza. Kulitokea matatizo makubwa kati ya wanawake hao watiwa mafuta. Tatizo lililokuwepo kati ya Euodia na Sintike lingeweza kuvuruga amani ya kutaniko lote. Biblia haituambii jinsi walivyoshughulikia hali hiyo, lakini inaelekea dada hao walikubali shauri lenye upendo kutoka kwa mtume Paulo. (Flp. 4:2, 3) Hali kama hizo zinaweza kusababisha matatizo katika makutaniko ya watu wa Yehova leo. Hata hivyo, matatizo kama hayo yanaweza kutatuliwa au kuepukwa tukitumia shauri linalopatikana katika Neno la Mungu, Biblia. Na ikiwa tunaheshimu sana Kitabu cha Yehova, tutaishi kulingana na maagizo yake.—Zab. 27:11. w16.11 3:1-3

Novemba 12-18
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha—2018 | Novemba

Novemba 12-18

MATENDO 1-3

  • Wimbo 104 na Sala

  • Utangulizi (Usizidi dak. 3)

HAZINA ZA NENO LA MUNGU

  • “Roho Takatifu Yamiminwa Juu ya Kutaniko la Kikristo”: (Dak. 10)

    • [Onyesha video ya Utangulizi wa Matendo.]

    • Mdo 2:1-8, 14, 37, 38, 41—Baada ya kupokea roho takatifu, wanafunzi wa Yesu walitoa ushahidi ambao ulifanya watu 3,000 hivi wabatizwe

    • Mdo 2:42-47—Wanafunzi wa Yesu walionyesha ukarimu mkubwa sana uliowaruhusu wageni waliobatizwa ambao walikuwa wametembelea Yerusalemu kubaki hapo kwa muda na kuimarisha imani yao (w86 12/1 29 ¶4-5, 7)

  • Kutafuta Hazina za Kiroho: (Dak. 8)

    • Mdo 3:15—Kwa nini Yesu anaitwa “Wakili Mkuu wa uzima”? (it-2 61 ¶1)

    • Mdo 3:19—Mstari huu unafafanuaje jinsi Yehova anavyosamehe watenda-dhambi wanaotubu? (cl 265 ¶14)

    • Usomaji wa Biblia wa juma hili umekufundisha nini kumhusu Yehova?

    • Ni hazina gani nyingine za kiroho ambazo ulipata katika usomaji wa Biblia wa juma hili?

  • Usomaji wa Biblia: (Usizidi dak. 4) Mdo 2:1-21

BORESHA HUDUMA YAKO

  • Ziara ya Kwanza: (Isizidi dak. 2) Tumia pendekezo la kuanzisha mazungumzo.

  • Video ya Ziara ya Kurudia ya Kwanza: (Dak. 5) Onyesha video, kisha zungumzeni kuihusu.

  • Hotuba: (Isizidi dak. 6) it-1 129 ¶2-3—Kichwa: Kwa Nini Mtu Alihitaji Kuchukua Mahali pa Yuda Lakini Si pa Mitume Wengine Waliokufa Wakiwa Waaminifu?

MAISHA YA MKRISTO

  • Wimbo 85

  • “Kushirikiana Kuhubiri Katika Eneo Lenye Lugha Mbalimbali”: (Dak. 15) Mazungumzo, itolewe na mwangalizi wa utumishi. Onyesha video, kisha zungumzeni kuihusu. Taja mipango ya kutaniko lenu kuhusu kuhubiri eneo lenye lugha nyingi.

  • Funzo la Biblia la Kutaniko: (Dak. 30) jy sura ya 43 ¶1-7

  • Pitia Mambo Makuu Ambayo Mmejifunza na Mtakayojifunza Juma Linalofuata (Dak. 3)

  • Wimbo 68 na Sala

Yaliyomo
Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2018 | Septemba

JUMA LA NOVEMBA 12-18, 2018

17 Wenye Furaha Ni Watu Wanaomtumikia “Mungu Mwenye Furaha”

Habari za Ziada

Makala nyingine katika gazeti hili

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki