Ezekieli
2 Kisha akaniambia: “Mwana wa binadamu,* simama kwa miguu yako ili nizungumuze na wewe.”+ 2 Wakati alizungumuza na mimi, roho ikaingia ndani yangu na kunifanya nisimame kwa miguu yangu+ ili niweze kumusikia Ule mwenye kuzungumuza na mimi.
3 Akaendelea kuniambia: “Mwana wa binadamu, ninakutuma kwa watu wa Israeli,+ kwa mataifa yenye kuasi ambayo yameniasi.+ Wao na mababu zao wamenikosea mupaka leo hii.+ 4 Ninakutuma kwa wana wenye kuwa kichwa-nguvu* na wenye moyo mugumu,+ na unapaswa kuwaambia, ‘Haya ndiyo mambo yenye Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.’ 5 Nao, kama watasikiliza ao watakataa kusikiliza—kwa maana wao ni nyumba yenye kuasi+—hakika watajua pia kwamba nabii alikuwa kati yao.+
6 “Lakini wewe, mwana wa binadamu, usiwaogope,+ na usiogope maneno yao, hata kama umezungukwa na michongoma na miiba*+ na unakaa kati ya nge. Usiogope maneno yao+ na usitishwe na nyuso zao,+ kwa maana wao ni nyumba yenye kuasi. 7 Unapaswa kuwaambia maneno yangu, kama watasikiliza ao hapana, kwa maana wao ni watu wenye kuasi.+
8 “Lakini wewe, mwana wa binadamu, sikiliza kile ninakuambia. Usikuwe muasi kama nyumba hii yenye kuasi. Fungua kinywa chako na ukule kile ninakupatia.”+
9 Wakati niliangalia, niliona mukono wenye ulikuwa umenyooshwa kunielekea,+ na katika mukono huo niliona kitabu cha kukunjwa chenye kuandikwa.+ 10 Wakati alikikunjua mbele yangu, kilikuwa kimeandikwa mbele na nyuma.+ Nyimbo za huzuni* na maombolezo na vilio vilikuwa vimeandikwa kwenye kitabu hicho.+