Zaburi
Muziki wa Daudi.
141 Ee Yehova, nimekuitia wewe.+
Ufanye haraka kuja kwangu.+
Utege sikio kwa sauti yangu ninapokuita.+
2 Sala yangu na itayarishwe kama uvumba+ mbele zako,+
Kuinuliwa kwa mikono yangu kama toleo la jioni la nafaka.+
3 Uweke mlinzi, Ee Yehova, kwa ajili ya kinywa changu;+
Uweke mwangalizi juu ya mlango wa midomo yangu.+
4 Usiuelekeze moyo wangu kwenye ubaya wowote,+
Ili kuendeleza matendo yenye sifa mbaya katika uovu+
Pamoja na watu wanaofanya mambo yenye kuumiza,+
Ili nisipate kujilisha vyakula vyao vitamu.+
5 Mwadilifu akinipiga, zingekuwa fadhili zenye upendo;+
Naye akinikaripia, hiyo ingekuwa mafuta juu ya kichwa,+
Ambayo kichwa changu hakingetaka kukataa.+
Kwa maana bado kungekuwako sala yangu wakati wa misiba yao.+
6 Waamuzi wao wametupwa chini kandokando ya mwamba,+
Lakini wameyasikia maneno yangu, kwamba ni yenye kupendeza.+
7 Kama mtu anavyoatua na kupasua kuni juu ya nchi,
8 Hata hivyo, macho yangu yanakuelekea wewe,+ Ee Yehova Bwana Mwenye Enzi Kuu.+
Nimekukimbilia.+
Usiimwage nafsi yangu.+