Marko
6 Naye akatoka huko na kuingia katika eneo lake la nyumbani, na wanafunzi wake wakamfuata.+ 2 Ilipofika siku ya sabato, akaanza kufundisha katika sinagogi; na hesabu kubwa zaidi ya wale waliokuwa wakisikiliza wakastaajabu na kusema: “Mtu huyu alipata wapi mambo haya?+ Na kwa nini mtu huyu apewe hekima hii, naye afanye matendo yenye nguvu hivyo kwa mikono yake? 3 Je, huyu si yule seremala+ mwana wa Maria+ na ndugu ya Yakobo+ na Yosefu na Yuda na Simoni?+ Na dada zake wapo hapa pamoja nasi, sivyo?” Kwa hiyo wakaanza kukwazika kwa sababu yake.+ 4 Lakini Yesu akaendelea kuwaambia: “Nabii hakosi kuheshimiwa ila katika eneo lake la nyumbani+ na katikati ya watu wa jamaa yake na katika nyumba yake mwenyewe.”+ 5 Kwa hiyo hakuweza kufanya matendo yenye nguvu huko ila kuweka mikono yake juu ya wagonjwa wachache na kuwaponya. 6 Kwa kweli, alistaajabia ukosefu wao wa imani. Naye akaenda akizunguka vijijini, akifundisha.+
7 Sasa akawaita wale kumi na wawili, akaanza kuwatuma wawili-wawili,+ naye akaanza kuwapa mamlaka juu ya roho wachafu.+ 8 Pia, akawaagiza wasichukue kitu chochote kwa ajili ya safari, wala mkate, wala mfuko wa chakula,+ wala pesa za shaba katika mikoba kwenye mishipi yao ila fimbo tu,+ 9 lakini wafunge viatu, na wasivae mavazi mawili ya ndani.+ 10 Zaidi ya hayo, akawaambia: “Popote mtakapoingia katika nyumba,+ kaeni humo mpaka mtakapoondoka.+ 11 Na mahali popote ambapo hamtapokewa wala kusikilizwa, mnapoondoka yakung’uteni mavumbi yaliyo chini ya miguu yenu ili kuwa ushahidi kwao.”+ 12 Kwa hiyo wakaondoka na kuhubiri ili watu wapate kutubu;+ 13 nao walikuwa wakitoa roho waovu+ wengi na kuwapaka mafuta+ watu wengi waliokuwa wagonjwa na kuwaponya.+
14 Basi Mfalme Herode akasikia, kwa maana jina la Yesu lilikuwa limejulikana na watu wote, na watu walikuwa wakisema: “Yohana mbatizaji amefufuliwa kutoka kwa wafu, na kwa sababu hiyo anatenda kazi zenye nguvu.”+ 15 Lakini wengine walikuwa wakisema: “Ni Eliya.”+ Bado wengine walikuwa wakisema: “Ni nabii kama mmoja wa manabii.”+ 16 Lakini Herode aliposikia hilo akaanza kusema: “Yohana ambaye nilimkata kichwa, ndiye huyo amefufuliwa.”+ 17 Kwa maana Herode mwenyewe alikuwa ametuma watu wakamkamata Yohana na kumfunga gerezani kwa sababu ya Herodia mke wa Filipo ndugu yake, kwa sababu Herode alikuwa amemwoa.+ 18 Kwa maana Yohana alikuwa amemwambia Herode tena na tena: “Si halali wewe kuwa na mke wa ndugu yako.”+ 19 Lakini Herodia alikuwa na kinyongo+ moyoni kumwelekea na alikuwa akitaka kumuua, lakini hakuweza.+ 20 Kwa maana Herode alikuwa akimwogopa+ Yohana, na alimjua kuwa mtu mwadilifu na mtakatifu;+ naye alikuwa akimlinda. Na baada ya kumsikia+ akawa hajui kabisa la kufanya, lakini aliendelea kumsikia kwa furaha.
21 Lakini siku inayofaa+ ikafika wakati Herode alipoandaa mlo wa jioni kwenye sikukuu ya kuzaliwa+ kwake kwa ajili ya wenye daraja la juu na viongozi wake wa kijeshi na walio wa cheo cha kwanza kabisa wa Galilaya. 22 Na binti ya Herodia huyohuyo akaingia, akacheza dansi na kumpendeza Herode na wale wenye kuketi+ pamoja naye. Mfalme akamwambia mwanamwali huyo: “Niombe chochote unachotaka, nami nitakupa.” 23 Ndiyo, akamwapia: “Chochote utakachoniomba, nitakupa hicho,+ hata nusu ya ufalme wangu.”+ 24 Naye akaenda akamwambia mama yake: “Niombe nini?” Akamwambia: “Kichwa cha Yohana mbatizaji.”+ 25 Mara akaingia haraka mpaka mahali alipokuwa mfalme na kutoa ombi lake, akisema: “Nataka unipe sasa hivi kwenye sahani kichwa cha Yohana Mbatizaji.” 26 Ijapokuwa mfalme alikuwa na huzuni sana, lakini hakutaka kumpuuza, kwa kufikiria vile viapo na wale waliokuwa wameketi mezani.+ 27 Kwa hiyo mara moja mfalme akamtuma mlinzi wa mfalme na kumwamuru akalete kichwa chake. Naye akaenda akamkata kichwa gerezani+ 28 akakileta kichwa chake kwenye sahani, naye akampa yule mwanamwali, naye mwanamwali akampa mama yake.+ 29 Wanafunzi wake waliposikia juu ya hilo wakaja wakachukua maiti yake na kuilaza katika kaburi.+
30 Nao mitume wakakusanyika pamoja mbele ya Yesu na kumwambia mambo yote waliyokuwa wamefanya na kufundisha.+ 31 Naye akawaambia: “Njooni, ninyi wenyewe, faraghani katika mahali pasipo na watu+ mpumzike kidogo.”+ Kwa maana watu walikuwa wakija na kwenda, nao hawakuwa hata na wakati wa kula mlo.+ 32 Kwa hiyo wakaenda zao wakiwa katika mashua wakawe peke yao katika mahali pasipo na watu.+ 33 Lakini watu wakawaona wakienda na wengi wakapata kujua hilo, na kutoka katika majiji yote wakakimbia pamoja kwenda huko kwa miguu na kufika mbele yao.+ 34 Basi, aliposhuka, akaona umati mkubwa, lakini akawasikitikia,+ kwa sababu walikuwa kama kondoo wasio na mchungaji.+ Naye akaanza kuwafundisha mambo mengi.+
35 Kufikia wakati huo saa ilikuwa imesonga sana, na wanafunzi wake wakamjia na kuanza kusema: “Mahali hapa hapana watu, na saa tayari imesonga sana.+ 36 Waache waende zao, ili waende mashambani na kwenye vijiji vinavyozunguka wakajinunulie chakula.”+ 37 Akajibu akawaambia: “Ninyi wapeni chakula.” Ndipo wakamwambia: “Je, twende tukanunue mikate yenye thamani ya dinari mia mbili na kuwapa watu ili wale?”+ 38 Akawaambia: “Mna mikate mingapi? Nendeni mkaone!” Baada ya kuhakikisha, wakasema: “Mitano, na samaki wawili.”+ 39 Naye akawaagiza watu wote waketi wakiwa vikundi-vikundi+ juu ya majani mabichi.+ 40 Nao wakajilaza chini katika vikundi vya watu 100 na vya watu 50.+ 41 Sasa akaichukua ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama juu mbinguni akatoa baraka,+ akaimega+ ile mikate na kuanza kuwapa wanafunzi, ili wapate kuiweka mbele ya watu hao; naye akawagawanya wale samaki wawili kwa ajili ya watu wote. 42 Kwa hiyo wote wakala, wakashiba;+ 43 nao wakaokota vipande, vikapu kumi na viwili vilivyojaa, mbali na wale samaki. 44 Zaidi ya hayo, wale waliokula ile mikate walikuwa wanaume elfu tano.+
45 Na, bila kukawia, akawaagiza wanafunzi wake waipande mashua na kumtangulia kwenda ukingo wa pili wa bahari kuelekea Bethsaida, huku yeye mwenyewe akiuruhusu umati uende.+ 46 Lakini baada ya kuwaaga akaenda mlimani ili asali.+ 47 Sasa ilipokuwa jioni, mashua ilikuwa katikati ya bahari, lakini yeye alikuwa peke yake kwenye nchi kavu.+ 48 Na alipowaona wakitaabika+ katika kuvuta kwao makasia, kwa maana upepo ulikuwa ukivuma kinyume chao, karibu kesha la nne la usiku akawaendea, akitembea juu ya bahari; lakini alitaka kuwapita. 49 Walipomwona akitembea juu ya bahari wakafikiri: “Ni mzuka!” nao wakapaaza sauti kubwa.+ 50 Kwa maana wote walimwona, wakataabika. Lakini mara moja akasema nao, naye akawaambia: “Jipeni moyo, ni mimi; msiogope.”+ 51 Naye akapanda na kuingia katika mashua pamoja nao, na upepo ukapungua. Ndipo wakashangaa sana ndani yao wenyewe,+ 52 kwa maana hawakuwa wamefahamu maana ya ile mikate, bali mioyo yao ilikuwa mizito isiweze kuelewa.+
53 Na walipovuka mpaka nchi kavu, wakaingia Genesareti na kutia meli nanga hapo karibu.+ 54 Lakini mara tu waliposhuka kutoka katika mashua, watu wakamtambua, 55 nao wakakimbia kuzunguka eneo lote hilo na kuanza kuwachukua huku na huku juu ya vitanda wale waliokuwa wakiugua mpaka kule walikosikia alikuwako. 56 Na kokote alikokuwa akiingia vijijini au majijini au mashambani+ walikuwa wakiweka wale wagonjwa sokoni, nao walikuwa wakiomba ili wapate kuugusa+ tu upindo+ wa vazi lake la nje. Na wote waliougusa wakapona.+