Waefeso
3 Kwa hiyo mimi, Paulo, mfungwa+ wa Kristo Yesu kwa ajili yenu, watu wa mataifa+— 2 ikiwa, kwa kweli, mmesikia juu ya usimamizi-nyumba+ wa fadhili zisizostahiliwa za Mungu ambao nilipewa kwa ajili yenu, 3 kwamba nilijulishwa siri takatifu kwa njia ya ufunuo,+ kama vile nilivyoandika kwa ufupi hapo mwanzoni. 4 Kwa kufikiria haya, mnapoisoma hii, mnaweza kuona utambuzi+ nilio nao katika siri takatifu+ ya Kristo. 5 Katika vizazi vingine siri hii+ haikujulishwa kwa wana wa binadamu kama vile ambavyo imefunuliwa+ sasa kwa mitume wake watakatifu na manabii+ kupitia roho, 6 yaani, kwamba watu wa mataifa wawe warithi wa pamoja na viungo vyenzi vya mwili+ na washiriki pamoja nasi wa ahadi+ katika muungano na Kristo Yesu kupitia habari njema. 7 Mimi nilikuja kuwa mhudumu+ wa hilo kulingana na zawadi ya bure ya fadhili zisizostahiliwa za Mungu nilizopewa kulingana na njia ambayo nguvu zake hutenda.+
8 Mimi, niliye mtu mdogo kuliko aliye mdogo+ zaidi kati ya watakatifu wote, nilipewa fadhili hizi zisizostahiliwa,+ ili niwatangazie mataifa+ habari njema juu ya utajiri+ usiopimika wa Kristo 9 na kufanya watu waone jinsi siri takatifu+ inavyosimamiwa+ ambayo tangu wakati uliopita usio na kipimo imefichwa katika Mungu, aliyeviumba vitu vyote.+ 10 Hiyo ilikuwa kwa kusudi kwamba sasa serikali na mamlaka+ zilizo katika mahali pa kimbingu zijulishwe kupitia kutaniko+ hekima ya Mungu ya namna nyingi sana,+ 11 kulingana na kusudi la milele alilofanyiza kuhusiana na Kristo,+ Yesu Bwana wetu, 12 ambaye kwa njia yake tuna uhuru huu wa kusema na tuna uwezo wa kukaribia+ tukiwa na uhakika kupitia imani yetu katika yeye. 13 Kwa hiyo nawaomba ninyi msife moyo kwa sababu ya hizi dhiki+ zangu kwa ajili yenu, kwa maana hizi zinamaanisha utukufu kwenu.
14 Kwa sababu hiyo nampigia Baba magoti,+ 15 ambaye kila familia+ mbinguni na duniani hupata jina kutokana naye,+ 16 kwa kusudi la kwamba awawezeshe ninyi kulingana na utajiri+ wa utukufu wake mfanywe kuwa na uwezo katika mtu mliye kwa ndani+ mkiwa na nguvu kupitia roho yake,+ 17 ili muwe na Kristo akikaa kupitia imani yenu katika mioyo yenu kwa upendo;+ ili mtie mizizi+ na kuimarishwa juu ya ule msingi,+ 18 ili mweze kufahamu kabisa akilini+ pamoja na watakatifu wote, upana na urefu na kimo na kina,+ 19 na kuujua upendo wa Kristo+ ambao unazidi ujuzi, ili mjawe na ujazo+ wote ambao Mungu hutoa.
20 Basi kwa yeye anayeweza, kulingana na nguvu zake zinazotenda+ ndani yetu, kufanya kwa wingi zaidi kupita mambo yote tunayoomba au tunayofikiri,+ 21 kwake kuwe na utukufu kwa njia ya kutaniko na kwa njia ya Kristo Yesu kwa vizazi vyote milele na milele.+ Amina.