1 Wathesalonike
4 Mwishowe, akina ndugu, tunawaomba ninyi na kuwahimiza kwa njia ya Bwana Yesu, kama vile mlivyopokea mafundisho kutoka kwetu kuhusu mnavyopaswa kutembea+ na kumpendeza Mungu, kwa kweli kama vile mnavyotembea, kwamba mwendelee kufanya hivyo kwa ukamili zaidi.+ 2 Kwa maana mnajua maagizo+ tuliyowapa ninyi kupitia Bwana Yesu.
3 Kwa maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu, kwamba mtakaswe,+ kwamba mjiepushe na uasherati;+ 4 kwamba kila mmoja wenu ajue jinsi ya kukiweza chombo chake+ mwenyewe katika utakaso+ na heshima, 5 si katika hamu yenye tamaa ya ngono+ kama ile waliyo nayo pia mataifa+ wale wasiomjua Mungu;+ 6 kwamba yeyote asifikie hatua ya kudhuru na kuziingilia haki za ndugu yake katika jambo hilo,+ kwa sababu Yehova ndiye anayelipiza adhabu kwa ajili ya mambo yote haya,+ kama vile tulivyowaambia ninyi kimbele na pia tukawapa ushahidi kamili.+ 7 Kwa maana Mungu alituita sisi bila kuruhusu nafasi ya uchafu, bali kuhusiana na utakaso.+ 8 Kwa hiyo, basi, mtu anayepuuza+ hampuuzi mwanadamu, bali Mungu,+ anayeitia roho yake takatifu+ ndani yenu.
9 Hata hivyo, kuhusu upendo wa kindugu,+ hamhitaji sisi tuwe tukiwaandikia ninyi, kwa maana ninyi wenyewe mmefundishwa na Mungu+ kupendana;+ 10 na, kwa kweli, mnafanya hivyo kwa ndugu wote katika Makedonia yote. Lakini tunawahimiza ninyi, akina ndugu, mwendelee kufanya hivyo kwa kipimo kamili zaidi, 11 na kufanya iwe shabaha yenu kuishi kwa utulivu+ na kukazia akili mambo yenu wenyewe+ na kufanya kazi kwa mikono yenu,+ kama vile tulivyowaagiza ninyi; 12 ili muwe mkijiendesha kwa adabu+ kuhusiana na watu walio nje+ na msiwe mkihitaji kitu chochote.+
13 Zaidi ya hayo, akina ndugu, hatutaki mkose kujua kuhusu wale walalao usingizi+ katika kifo; ili msiwe na huzuni kama wale watu wengine wasio na tumaini.+ 14 Kwa maana ikiwa imani yetu ni kwamba Yesu alikufa na kufufuliwa tena,+ vivyo hivyo pia, wale ambao wamelala usingizi katika kifo kupitia Yesu, Mungu atawaleta pamoja naye.+ 15 Kwa maana tunawaambia hivi kwa neno la Yehova,+ kwamba sisi tulio hai ambao tutabaki mpaka kuwapo kwa Bwana+ hatutawatangulia kwa vyovyote wale ambao wamelala usingizi katika kifo; 16 kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni+ akiwa na mwito wenye amri, kwa sauti ya malaika mkuu+ na kwa tarumbeta+ ya Mungu, na wale walio wafu katika muungano na Kristo watafufuliwa kwanza.+ 17 Baadaye sisi tulio hai tuliobaki tutanyakuliwa,+ pamoja nao,+ katika mawingu+ ili kukutana+ na Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana sikuzote.+ 18 Kwa hiyo endeleeni kufarijiana kwa maneno hayo.