33 Kwa maana Tofethi+ yake imepangwa kuanzia majuzi; pia imetayarishwa kwa ajili ya mfalme mwenyewe.+ Yeye amefanya fungu lake liwe na kina kirefu. Kuna moto na kuni kwa wingi. Pumzi ya Yehova, kama mto wa kiberiti, inawaka juu yake.+
31 Nao wamejenga mahali pa juu pa Tofethi,+ palipo katika bonde la mwana wa Hinomu,+ ili kuwateketeza wana wao na binti zao katika moto,+ jambo ambalo sikuamuru wala halikuingia moyoni mwangu.’+
6 “‘“Kwa hiyo, tazama! kuna siku zinakuja,” asema Yehova, “wakati mahali hapa hapataitwa tena Tofethi+ na bonde la mwana wa Hinomu,+ bali bonde la uuaji.
11 Nawe uwaambie, ‘Yehova wa majeshi amesema hivi: “Ndivyo nitakavyowavunja watu hawa na jiji hili kama mtu anavyokivunja chombo cha mfinyanzi hivi kwamba hakiwezi kurekebishwa tena;+ nao watazika katika Tofethi+ mpaka pasiwe na mahali zaidi pa kuzikia.”’+