Isaya
30 “Ole wao wana wakaidi,”+ asema Yehova, “wale walio na mwelekeo wa kutekeleza shauri, lakini si la kutoka kwangu;+ na kumimina toleo la kinywaji, lakini si kwa roho yangu, ili kuongeza dhambi juu ya dhambi;+ 2 wale wanaojitayarisha kushuka kwenda Misri+ na ambao hawakuuliza kutoka kinywani mwangu,+ ili kupata kinga katika ngome ya Farao na kupata kimbilio katika kivuli cha Misri!+ 3 Na ngome ya Farao itakuwa kwenu sababu ya kuona aibu,+ na kimbilio katika kivuli cha Misri sababu ya kufedheheka.+ 4 Kwa maana wakuu wake wamekuja kuwa katika Soani,+ na wajumbe wake wamefika hata Hanesi. 5 Kila mtu hakika atakionea aibu kikundi cha watu ambacho hakimletei mtu faida, ambacho hakina msaada wala hakileti faida, lakini husababisha aibu na pia husababisha shutuma.”+
6 Tangazo juu ya wanyama wa kusini:+ Katika nchi ya taabu na hali ngumu,+ ya simba na chui anayenguruma, ya kipiri na nyoka wa moto anayeruka,+ juu ya mabega ya punda wakomavu wanabeba mali zao, na akiba zao juu ya nundu za ngamia.+ Havitakuwa na faida kwa ajili ya watu. 7 Na Wamisri ni ubatili mtupu, nao watasaidia bure tu.+ Kwa hiyo nimemwita huyu: “Rahabu+—kazi yao ni kuketi tuli.”
8 “Sasa njoo, iandike juu ya bamba pamoja nao, na uiandike katika kitabu,+ ili itumike kwa ajili ya siku ya baadaye, kuwa ushahidi mpaka wakati usio na kipimo.+ 9 Kwa maana wao ni watu waasi,+ wana wasiosema kweli,+ wana ambao hawataki kuisikia sheria ya Yehova;+ 10 ambao wamewaambia wale wanaoona, ‘Msione,’ na wale wanaopata maono, ‘Msione maono ya mambo manyoofu kwa ajili yetu.+ Tuambieni mambo laini; oneni maono ya mambo ya udanganyifu.+ 11 Geukeni kando kutoka njiani; ondokeni katika pito.+ Mkomesheni Mtakatifu wa Israeli kwa ajili yetu.’”+
12 Kwa hiyo Mtakatifu wa Israeli amesema hivi: “Kwa sababu ya ninyi kulikataa neno hili,+ na kwa kuwa mnategemea upunjaji na yaliyo ya hila na ninyi mnajitegemeza juu yake,+ 13 kwa hiyo kosa hili litakuwa kwenu kama sehemu iliyovunjika ambayo inakaribia kuanguka, uvimbe katika ukuta ulioinuliwa juu sana,+ ambao kubomoka kwake kunaweza kuja kwa ghafula, mara moja.+ 14 Na hakika mtu atauvunja kama vile mtungi mkubwa wa wafinyanzi unavyovunjwa,+ kupondwa vipande-vipande bila mtu kuuachilia, hivi kwamba kati ya vipande vyake vilivyopondwa hakuwezi kupatikana kigae kinachoweza kutumiwa kukusanya moto jikoni wala kuteka maji kutoka eneo lenye matope.”+
15 Kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, Mtakatifu wa Israeli,+ amesema hivi: “Mkirudi na kupumzika mtaokolewa. Nguvu zenu zitakuwa tu katika kukaa bila usumbufu na katika kutegemea.”+ Lakini hamkutaka.+ 16 Nanyi mkasema: “Hapana, bali tutakimbia juu ya farasi!”+ Ndiyo sababu mtakimbia. “Nasi tutapanda juu ya farasi wepesi!”+ Ndiyo sababu wale wanaowafuatilia ninyi watajionyesha kuwa wepesi.+ 17 Watu elfu moja watatetemeka kwa sababu ya kemeo la mmoja;+ mtakimbia kwa sababu ya kemeo la watano mpaka mtakapokuwa mmebaki kama mlingoti juu ya kilele cha mlima na kama ishara juu ya kilima.+
18 Na kwa hiyo Yehova ataendelea kutarajia kuwaonyesha ninyi kibali,+ na kwa hiyo atasimama ili kuwaonyesha ninyi rehema.+ Kwa maana Yehova ni Mungu wa hukumu.+ Wenye furaha+ ni wale wote wanaoendelea kumtarajia.+ 19 Wakati watu walio katika Sayuni+ watakapokaa katika Yerusalemu,+ wewe hutalia kwa vyovyote.+ Yeye hakika atakuonyesha kibali unapotoa sauti ya kilio chako; mara tu atakapokisikia kwa kweli atakujibu.+ 20 Na Yehova hakika atawapa ninyi mkate kwa namna ya taabu na maji kwa namna ya ukandamizaji;+ na bado Mfundishaji wako Mkuu hatajificha tena, na macho yako yatakuwa macho yanayomwona Mfundishaji Mkuu wako.+ 21 Na masikio yako yatasikia neno nyuma yako likisema: “Hii ndiyo njia.+ Tembeeni ndani yake,” iwe mtakwenda upande wa kuume au iwe mtakwenda upande wa kushoto.+
22 Nanyi mtakitia unajisi kifuniko cha sanamu zenu za kuchongwa za fedha+ na kifuniko kinachobana cha sanamu yenu ya kuyeyushwa+ ya dhahabu.+ Utazitawanya.+ Kama mwanamke mwenye hedhi, utaiambia hivi: “Uchafu mtupu!”+ 23 Naye hakika ataleta mvua kwa ajili ya mbegu yako unayoipanda katika udongo,+ na mkate kuwa mazao ya udongo, ambao utakuwa mnono na wenye mafuta.+ Mifugo yako italisha katika siku hiyo katika malisho mapana.+ 24 Na ng’ombe na punda wakomavu wanaolima udongo watakula chakula kilichokolezwa kwa mboga chungu, ambacho kilipepetwa kwa sepetu+ na kwa uma. 25 Na juu ya kila mlima mrefu na juu ya kila kilima kirefu kutakuja kuwa na vijito,+ mitaro ya maji, katika siku ile ya mauaji makubwa wakati minara itakapoanguka.+ 26 Na nuru ya mwezi mpevu itakuwa kama nuru ya jua linaloangaza; na ile nuru ya jua linaloangaza itaongezeka mara saba,+ kama nuru ya siku saba, siku ile Yehova atakapofunga mvunjiko+ wa watu wake na kuliponya+ jeraha kali linalotokana na pigo kutoka kwake.
27 Tazama! Jina la Yehova linakuja kutoka mbali, likiwaka kwa hasira+ yake na kwa mawingu mazito. Na midomo yake imejaa shutuma, na ulimi wake ni kama moto unaoteketeza.+ 28 Na roho yake ni kama mto unaofurika ambao hufika mpaka shingoni,+ ili kuyarusha mataifa huku na huku kwa kichujio+ cha ubatili; na lijamu+ inayomfanya mtu kwenda huku na huku itakuwa katika taya za vikundi vya watu.+ 29 Ninyi mtakuwa na wimbo+ kama ule wakati wa usiku ambapo mtu hujitakasa kwa ajili ya sherehe,+ na kushangilia kwa moyo kama kule kwa mtu anayetembea akiwa na filimbi+ ili kuingia katika mlima wa Yehova,+ kwa Mwamba wa Israeli.+
30 Na Yehova hakika atafanya utukufu wa sauti+ yake usikiwe naye atafanya kushuka kwa mkono wake kuonekane,+ katika kuwaka kwa hasira+ na mwali wa moto unaoteketeza+ na tufani ya mvua na dhoruba ya mvua+ na mawe ya mvua.+ 31 Kwa maana Ashuru itaingiwa na woga kwa sababu ya sauti ya Yehova;+ yeye ataipiga kwa fimbo.+ 32 Na kila pigo la fimbo yake ya kutia adabu ambayo Yehova atafanya itue juu ya Ashuru hakika litakuwa pamoja na matari na vinubi;+ naye kwa kweli atapiga vita juu yao kwa mtikiso wa silaha za vita.+ 33 Kwa maana Tofethi+ yake imepangwa kuanzia majuzi; pia imetayarishwa kwa ajili ya mfalme mwenyewe.+ Yeye amefanya fungu lake liwe na kina kirefu. Kuna moto na kuni kwa wingi. Pumzi ya Yehova, kama mto wa kiberiti, inawaka juu yake.+