Mwanzo
8 Kisha Mungu akamkumbuka+ Noa na kila mnyama-mwitu na kila mnyama wa kufugwa ambaye alikuwa pamoja naye ndani ya safina.+ Mungu akafanya upepo upite juu ya dunia, nayo maji yakaanza kupungua.+ 2 Nazo chemchemi za kilindi cha maji+ na malango+ ya mbinguni zikafungwa, na kwa hiyo mvua kubwa kutoka mbinguni ikazuiliwa. 3 Nayo maji yakaanza kupungua kutoka juu ya dunia, yakapungua hatua kwa hatua; na mwishoni mwa siku 150 maji hayakuwapo.+ 4 Katika mwezi wa saba, siku ya kumi na saba ya mwezi, safina+ ikatua kwenye milima ya Ararati.+ 5 Na maji yakazidi kupungua hatua kwa hatua mpaka mwezi wa kumi. Katika mwezi wa kumi, siku ya kwanza ya mwezi, vilele vya milima vikaonekana.+
6 Basi ikawa kwamba mwishoni mwa siku 40 Noa akafungua dirisha+ la safina ambalo alikuwa amelifanyiza. 7 Baada ya hapo akatuma kunguru,+ naye akaruka-ruka nje, akienda na kurudi, mpaka maji yalipokauka kutoka juu ya dunia.
8 Baadaye akatuma njiwa+ nje ili kuona ikiwa maji yalikuwa yamepungua kutoka katika uso wa nchi. 9 Na yule njiwa hakupata mahali popote pa kupumzisha wayo wa mguu wake. Basi akamrudia katika safina kwa sababu bado maji yalikuwako juu ya uso wa dunia yote.+ Kwa hiyo akaunyoosha mkono wake na kumchukua. Akamwingiza ndani ya safina. 10 Naye akaendelea kungoja siku saba tena, na mara nyingine tena akamtuma yule njiwa nje ya safina. 11 Baadaye yule njiwa akamjia karibu na wakati wa jioni na, tazama! jani bichi la mzeituni+ lilikuwa katika mdomo wake. Basi Noa akajua kwamba maji yalikuwa yamepungua kutoka juu ya dunia.+ 12 Naye akaendelea kungoja siku saba tena. Ndipo akamtuma yule njiwa, lakini hakurudi kwake tena kamwe.+
13 Basi katika mwaka wa mia sita na moja,+ mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya mwezi, ikawa kwamba maji yalikuwa yamepungua kutoka juu ya dunia; Noa akakiondoa kifuniko cha safina akaona, na tazama, uso wa nchi ulikuwa umekauka kabisa.+ 14 Na katika mwezi wa pili, siku ya 27 ya mwezi, dunia ilikuwa imekauka.+
15 Sasa Mungu akasema na Noa, akamwambia: 16 “Toka nje ya safina, wewe na mke wako na wana wako na wake za wana wako pamoja nawe.+ 17 Kila kiumbe hai kilicho pamoja nawe chenye mwili wa kila namna,+ kati ya viumbe vinavyoruka+ na kati ya wanyama+ na kati ya wanyama wote wanaotembea ambao hutembea juu ya dunia,+ toka nao nje, kwa kuwa wanapaswa kujaa duniani, wazaane na kuwa wengi duniani.”+
18 Ndipo Noa akatoka nje, na wanawe+ pia na mke wake na wake za wanawe pamoja naye. 19 Kila kiumbe hai, kila mnyama anayetembea na kila kiumbe kinachoruka, kila kitu kinachotembea juu ya dunia, kulingana na familia zao walitoka nje ya safina.+ 20 Noa akamjengea Yehova madhabahu+ na kuchukua baadhi ya wanyama wote walio safi+ na baadhi ya viumbe vyote vinavyoruka ambavyo ni safi,+ akatoa matoleo ya kuteketezwa juu ya ile madhabahu.+ 21 Na Yehova akaanza kunusa harufu ya kutuliza,+ na kwa hiyo Yehova akasema moyoni mwake:+ “Sitailaani nchi+ tena kamwe kwa sababu ya mwanadamu, kwani mwelekeo+ wa moyo wa mwanadamu ni mbaya tangu ujana wake na kuendelea;+ nami sitakipiga tena kamwe kila kitu chenye uhai kama vile nilivyofanya.+ 22 Siku zote ambazo dunia inaendelea kuwapo, kupanda mbegu na kuvuna, baridi na joto, majira ya kiangazi na majira ya baridi kali, mchana na usiku, havitakoma kamwe.”+