Zaburi
Mshukuruni Yehova, kwa maana yeye ni mwema;+
Kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo.+
2 Ni nani anayeweza kuyasema matendo yenye nguvu ya Yehova,+
Au anayeweza kufanya sifa yake yote isikiwe?+
4 Unikumbuke, Ee Yehova, kwa nia njema kuelekea watu wako.+
Unitunze kwa wokovu wako,+
5 Ili nipate kuona wema kwa wachaguliwa wako,+
Ili nipate kushangilia kwa shangwe ya taifa lako,+
Ili nipate kujisifu pamoja na urithi wako.+
7 Mababu zetu huko Misri,
Hawakuonyesha ufahamu wowote katika kazi zako za ajabu.+
Hawakukumbuka wingi wa fadhili zako kuu zenye upendo,+
Bali walijiendesha kwa uasi penye bahari, kando ya Bahari Nyekundu.+
9 Kwa hiyo akaikemea Bahari Nyekundu, nayo ikakauka hatua kwa hatua;+
Naye akawatembeza kupita katika kilindi cha maji kana kwamba ni nyikani;+
10 Na kwa hiyo akawaokoa kutoka katika mkono wa mchukiaji+
Na kuwakomboa kutoka katika mkono wa adui.+
19 Na zaidi ya hayo, wakatengeneza ndama katika Horebu+
Na kuinamia sanamu ya kuyeyushwa,+
20 Hivi kwamba wakabadili utukufu wangu+
Kwa ajili ya mfano wa ng’ombe mwenye kula majani.+
21 Walimsahau Mungu Mwokozi wao,+
Mtendaji wa mambo makuu nchini Misri,+
22 Kazi za ajabu katika nchi ya Hamu,+
Mambo yenye kuogopesha kwenye Bahari Nyekundu.+
23 Naye alikuwa karibu kusema waangamizwe,+
Isingalikuwa ni kwa sababu ya Musa mchaguliwa wake,
Aliyesimama penye mwanya mbele zake,+
Ili kuigeuza ghadhabu yake asiwaharibu.+
26 Kwa hiyo akainua mkono wake katika kiapo juu yao,+
Kwamba angewafanya waanguke nyikani,+
27 Na kwamba angefanya uzao wao uanguke kati ya mataifa,+
Na kwamba angewatawanya katika nchi mbalimbali.+
32 Tena, wakafanya uchokozi katika maji ya Meriba,+
Hivi kwamba mambo yakamwendea Musa vibaya kwa sababu yao.+
38 Kwa hiyo wakaendelea kumwaga damu isiyo na hatia,+
Damu ya wana wao na binti zao,
Ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani;+
Na nchi ikachafuliwa na umwagaji wa damu.+
41 Naye akawatia mkononi mwa mataifa tena na tena,+
Ili wale wanaowachukia wapate kutawala juu yao,+
42 Na ili adui zao wapate kuwakandamiza,
Na ili wapate kutiishwa chini ya mkono wao.+
Lakini wao wakawa wakijiendesha kwa uasi katika mwendo wao wa kutokutii,+
Nao wakashushwa kwa sababu ya kosa lao.+
45 Naye akalikumbuka agano lake juu yao,+
Naye akajuta kulingana na wingi wa fadhili zake kuu zenye upendo.+