Luka
9 Ndipo akawaita pamoja wale kumi na wawili, akawapa nguvu na mamlaka juu ya roho wote waovu na za kuponya magonjwa.+ 2 Na kwa hiyo akawatuma kuhubiri ufalme wa Mungu na kuponya, 3 naye akawaambia: “Msichukue kitu chochote kwa ajili ya safari, wala fimbo wala mfuko wa chakula, wala mkate wala fedha; wala msiwe na mavazi mawili ya ndani.+ 4 Lakini popote mtakapoingia katika nyumba, kaeni humo na mwondoke humo.+ 5 Na popote ambapo watu hawawapokei ninyi, mnapoondoka katika jiji hilo+ yakung’uteni mavumbi kutoka miguuni penu ili kuwa ushahidi juu yao.”+ 6 Ndipo walipoanza kuondoka wakapita katika eneo hilo kutoka kijiji mpaka kijiji, wakitangaza habari njema na kuponya kila mahali.+
7 Sasa Herode mtawala wa wilaya akasikia juu ya mambo yote yaliyokuwa yakitukia, naye akafadhaika sana kwa sababu baadhi ya watu walikuwa wakisema kwamba Yohana alikuwa amefufuliwa kutoka kwa wafu,+ 8 lakini wengine kwamba Eliya alikuwa ameonekana, na bado wengine kwamba mtu fulani mmoja wa manabii wa kale alikuwa amefufuliwa. 9 Herode akasema: “Yohana nilimkata kichwa.+ Basi, ni nani huyu ambaye juu yake ninasikia mambo ya namna hiyo?” Kwa hiyo alikuwa akitafuta+ kumwona.
10 Na mitume waliporudi wakamsimulia mambo waliyokuwa wameyafanya.+ Ndipo akawachukua waambatane naye, nao wakaondoka kwenda faraghani+ na kuingia katika jiji linaloitwa Bethsaida. 11 Lakini umati ulipojua, ukamfuata. Naye akawapokea kwa fadhili na kuanza kuwaambia juu ya ufalme wa Mungu,+ naye akawaponya wale wanaohitaji kuponywa.+ 12 Ndipo mchana ukaanza kushuka. Wale kumi na wawili sasa wakaja na kumwambia: “Waambie umati waondoke, waende vijijini na upande wa mashambani wenye kuzunguka na kujipatia makao na wapate chakula, kwa sababu huku nje sisi tuko katika mahali pasipo na watu.”+ 13 Lakini akawaambia: “Ninyi wapeni chakula.”+ Wakasema: “Sisi hatuna kitu zaidi ya mikate mitano na samaki wawili,+ isipokuwa labda sisi wenyewe twende na kununua vyakula kwa ajili ya watu wote hawa.”+ 14 Kwa kweli, walikuwa karibu wanaume 5,000.+ Lakini akawaambia wanafunzi wake: “Waagizeni waketi kama kwenye milo, vikundi-vikundi vya karibu 50 kila kimoja.”+ 15 Nao wakafanya hivyo na kuwaketisha wote. 16 Ndipo akichukua ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama juu mbinguni, akavibariki na kuvimega, akaanza kuwapa wanafunzi waviweke mbele ya umati.+ 17 Kwa hiyo wote wakala, wakashiba, na ziada waliyokuwa nayo ikaokotwa, vikapu kumi na viwili vya vipande.+
18 Baadaye, alipokuwa akisali peke yake, wanafunzi walimjia pamoja, naye akawauliza, akisema: “Umati unasema mimi ni nani?”+ 19 Wakajibu wakasema: “Yohana Mbatizaji; lakini wengine, Eliya, na wengine bado, kwamba mmoja wa manabii wa kale amefufuliwa.”+ 20 Ndipo akawaambia: “Ingawa hivyo, ninyi mnasema mimi ni nani?” Petro akajibu, akasema:+ “Kristo+ wa Mungu.” 21 Ndipo akawaagiza kwa kusisitiza wasimwambie mtu yeyote jambo hilo,+ 22 lakini akasema: “Mwana wa binadamu lazima apatwe na mateso mengi na kukataliwa na wanaume wazee na wakuu wa makuhani na waandishi, na kuuawa,+ na siku ya tatu afufuliwe.”+
23 Ndipo akaendelea kuwaambia wote: “Mtu yeyote akitaka kunifuata, na ajikane+ mwenyewe na kuuchukua mti wake wa mateso siku baada ya siku na kunifuata sikuzote.+ 24 Kwa maana yeyote yule anayetaka kuiokoa nafsi yake ataipoteza; lakini yeyote yule anayeipoteza nafsi yake kwa ajili yangu ndiye atakayeiokoa.+ 25 Kwa kweli, mtu anapata faida gani ikiwa anaupata ulimwengu wote lakini aipoteze nafsi yake mwenyewe au apate hasara?+ 26 Kwa maana mtu yeyote yule atakayenionea aibu mimi na maneno yangu, Mwana wa binadamu atamwonea aibu mtu huyo atakapofika katika utukufu wake na ule wa Baba na wa malaika watakatifu.+ 27 Lakini ninawaambia ninyi kwa kweli, Kuna baadhi ya wale wanaosimama hapa ambao hawataonja kifo kamwe mpaka kwanza wauone ufalme wa Mungu.”+
28 Kwa kweli, karibu siku nane baada ya maneno hayo, aliambatana na Petro na Yohana na Yakobo wakapanda mlimani ili kusali.+ 29 Naye alipokuwa akisali sura ya uso+ wake ikawa tofauti na vazi lake likawa jeupe kwa kumetameta.+ 30 Pia, tazama! wanaume wawili walikuwa wakiongea naye, Musa na Eliya.+ 31 Hawa walitokea wakiwa na utukufu nao wakaanza kuongea juu ya kuondoka kwake ambako angetimiza huko Yerusalemu.+ 32 Sasa Petro na wale waliokuwa pamoja naye walikuwa wamelemewa na usingizi; lakini walipopata kuamka kabisa waliuona utukufu+ wake na wale wanaume wawili waliosimama pamoja naye. 33 Nao walipokuwa wakitengwa kutoka kwake, Petro akamwambia Yesu: “Mwalimu, ni vizuri kwetu kuwa hapa, kwa hiyo na tusimamishe mahema matatu, moja lako na moja la Musa na moja la Eliya,” naye hakuwa akitambua alilokuwa akisema.+ 34 Lakini alipokuwa akisema mambo haya wingu likatokea na kuanza kuwafunika. Walipokuwa wakiingia katika wingu, wakaogopa.+ 35 Na sauti ikatoka katika lile wingu,+ ikisema: “Huyu ni Mwanangu, ambaye amechaguliwa.+ Msikilizeni.”+ 36 Na ile sauti ilipokuwa ikitokea Yesu alionekana akiwa peke yake.+ Lakini wakaendelea kukaa kimya nao hawakumwambia yeyote siku hizo lolote kati ya mambo waliyoona.+
37 Siku iliyofuata, waliposhuka kutoka mlimani, umati mkubwa ulikutana naye.+ 38 Na, tazama! mwanamume mmoja akapaaza sauti kutoka katika umati, akisema: “Mwalimu, ninakuomba umtazame kidogo mwanangu, kwa sababu yeye ni mzaliwa-pekee+ wangu, 39 na, tazama! roho+ humchukua, na kwa ghafula yeye hupaaza sauti, na huyo roho humfanya agaegae pamoja na kutoa povu, naye hamwachi kabisa baada ya kumchubua. 40 Nami niliwaomba wanafunzi wako wamfukuze roho huyo, lakini hawakuweza.”+ 41 Yesu akajibu akasema: “Enyi kizazi kisicho na imani na kilichopotoka,+ nitaendelea kuwa pamoja nanyi na kuwavumilia ninyi mpaka wakati gani? Mlete hapa mwana wako.”+ 42 Lakini hata alipokuwa akikaribia, yule roho mwovu akamwangusha chini na kumfanya agaegae kwa nguvu nyingi. Hata hivyo, Yesu akamkemea yule roho mchafu na kumponya mvulana naye akamkabidhi baba yake.+ 43 Basi, wote wakaanza kustaajabishwa na nguvu+ kuu za Mungu.
Sasa walipokuwa wote wakistaajabia mambo yote aliyokuwa akifanya, akawaambia wanafunzi wake: 44 “Yawekeni maneno hayo katika masikio yenu, kwa maana Mwana wa binadamu atatiwa mikononi mwa watu.”+ 45 Lakini wao wakashindwa kuelewa maneno hayo. Kwa kweli, yalifichwa ili wasipate kuyafahamu, nao waliogopa kumuuliza juu ya maneno hayo.+
46 Ndipo wakaanza kujadiliana kati yao kuhusu ni nani angekuwa mkuu zaidi kati yao.+ 47 Yesu, akijua mawazo ya mioyo yao, akachukua mtoto mchanga, akamweka kando yake+ 48 na kuwaambia: “Yeyote yule anayempokea mtoto huyu mchanga kwa msingi wa jina langu ananipokea mimi pia, na yeyote anayenipokea, anampokea pia yule aliyenituma.+ Kwa maana anayejiendesha kama aliye mdogo+ zaidi kati yenu nyote ndiye aliye mkuu.”+
49 Yohana akajibu akasema: “Mwalimu, tulimwona mtu fulani akitoa roho waovu+ kwa kutumia jina lako nasi tukajaribu kumzuia,+ kwa sababu hafuatani nasi.”+ 50 Lakini Yesu akamwambia: “Msijaribu kumzuia, kwa maana yule ambaye hayuko kinyume chenu yuko upande wenu.”+
51 Sasa siku zilipokuwa zikikamilika ili yeye achukuliwe juu,+ aliukaza uso wake kwenda Yerusalemu. 52 Kwa hiyo akatuma wajumbe kumtangulia. Nao wakaenda na kuingia katika kijiji cha Wasamaria,+ kumfanyia matayarisho; 53 lakini hawakumpokea, kwa sababu uso wake ulikuwa umekazwa kwenda Yerusalemu.+ 54 Wanafunzi Yakobo na Yohana+ walipoona hilo wakasema: “Bwana, je, unataka tuuambie moto+ ushuke kutoka mbinguni na kuwaangamiza?” 55 Lakini akageuka akawakemea. 56 Basi wakaenda kwenye kijiji tofauti.
57 Sasa walipokuwa wakienda barabarani, mtu fulani akamwambia: “Nitakufuata popote ambapo utaenda.”+ 58 Naye Yesu akamwambia: “Mbweha wana mapango na ndege wa mbinguni wana viota, lakini Mwana wa binadamu hana mahali popote pa kulaza kichwa chake.”+ 59 Ndipo akamwambia mwingine: “Uwe mfuasi wangu.” Mtu huyo akasema: “Niruhusu kwanza niondoke nikamzike baba yangu.”+ 60 Lakini akamwambia: “Waache wafu+ wawazike wafu wao, lakini wewe nenda zako ukautangaze kotekote ufalme wa Mungu.”+ 61 Na bado mwingine akasema: “Nitakufuata, Bwana; lakini kwanza niruhusu niwaage+ watu wa nyumbani mwangu.” 62 Yesu akamwambia: “Hakuna mtu ambaye ameweka mkono wake kwenye jembe la ng’ombe+ na kutazama mambo yaliyo nyuma+ anayefaa kwa ajili ya ufalme wa Mungu.”