Isaya
57 Mwadilifu ameangamia,+ lakini hakuna anayeweka jambo hilo moyoni.+ Na watu wa fadhili zenye upendo wanakusanywa kwa wafu,+ hali hakuna anayetambua kuwa ni kwa sababu ya msiba kwamba mwadilifu amekusanywa.+ 2 Yeye huingia katika amani;+ wao hupumzika+ vitandani+ mwao, kila mmoja anayetembea kwa unyoofu.+
3 “Na kwa habari yenu, njooni karibu hapa,+ ninyi wana wa mwanamke mwenye kubashiri,+ uzao wa mzinzi na wa mwanamke anayefanya ukahaba:+ 4 Mnajifurahisha juu ya nani?+ Mnaendelea kufungua wazi kinywa, na kutoa ulimi,+ juu ya nani? Je, ninyi si watoto wa ukosaji, uzao wa uwongo,+ 5 wale wanaojiwasha tamaa kati ya miti mikubwa,+ chini ya kila mti wenye majani mengi,+ wakiwaua watoto katika mabonde ya mito chini ya mipasuko ya miamba?+
6 “Fungu lako lilikuwa pamoja na mawe laini ya bonde la mto.+ Hayo—hayo yalikuwa kura yako.+ Zaidi ya hayo, uliyamwagia toleo la kinywaji,+ ulitoa zawadi. Je, nitajifariji kwa mambo hayo?+ 7 Uliweka kitanda chako juu ya mlima mrefu na ulioinuka.+ Ulienda hapo pia kutoa dhabihu.+ 8 Nawe uliweka ukumbusho wako nyuma ya mlango na ya mwimo wa mlango.+ Kwa maana uliniacha, ukajifunua na kupanda juu; ulikipanua kitanda chako.+ Nawe ukafanya agano pamoja nao kwa ajili yako. Ulipenda kuwa nao kitandani.+ Ulikitazama kiungo cha uume. 9 Nawe uliteremka kumwendea Meleki ukiwa na mafuta, na ukaendelea kufanya marhamu yako kuwa mengi.+ Nawe ukaendelea kuwatuma mbali wajumbe wako, hivi kwamba ukashusha mambo mpaka katika Kaburi.*+ 10 Umefanya kazi katika wingi wa njia zako.+ Hukusema, ‘Hakuna matumaini!’ Umepata kitu cha kuhuisha nguvu zako.+ Ndiyo sababu hujawa mgonjwa.+
11 “Ulimhofu na kuanza kumwogopa nani,+ hivi kwamba ukaanza kusema uwongo?+ Lakini wewe hukunikumbuka mimi.+ Hukuweka moyoni mwako jambo lolote.+ Je, mimi sikuwa nikinyamaza kimya na kuficha mambo?+ Kwa hiyo hukuniogopa mimi.+ 12 Mimi mwenyewe nitatangaza uadilifu+ wako na kazi+ zako, kwamba hazitakupa faida.+ 13 Wakati unapotoa kilio cha kuomba msaada vitu vyako ulivyokusanya havitakukomboa,+ bali upepo utavichukulia mbali vyote.+ Pumzi itaviondolea mbali, lakini yule anayenikimbilia+ atairithi nchi naye ataumiliki mlima wangu mtakatifu.+ 14 Na hakika mtu atasema, ‘Fanyeni matuta, fanyeni matuta! Fungueni njia.+ Ondoeni kipingamizi chochote katika njia ya watu wangu.’”+
15 Kwa maana Yeye Aliye Juu na Aliyeinuka Sana,+ anayeishi milele+ na ambaye jina lake ni takatifu,+ amesema hivi: “Mimi ninakaa kileleni na katika mahali patakatifu,+ pia pamoja na mtu aliyepondwa na mwenye roho ya unyenyekevu,+ ili kuipa uhai roho ya watu wa hali ya chini na kuupa uhai moyo wa wale wanaopondwa.+ 16 Kwa maana sitashindana mpaka wakati usio na kipimo, wala sitakuwa na ghadhabu daima;+ kwa maana roho itafifia+ kwa sababu yangu, viumbe vinavyopumua ambavyo mimi mwenyewe nimevifanya.+
17 “Nilikuwa na ghadhabu kutokana na makosa ya pato lake lisilo la haki,+ nami nikampiga, nikiuficha uso wangu,+ nilipokuwa na ghadhabu. Lakini yeye aliendelea kutembea akiwa mwasi+ katika njia ya moyo wake. 18 Nimeziona njia zake; nami nikaanza kumponya+ na kumwelekeza+ na kumlipa yeye malipo kwa faraja+ na watu wake wanaoomboleza.”+
19 “Mimi ninaumba matunda ya midomo.+ Kutakuwa na amani yenye kuendelea kwa yule aliye mbali na kwa yule aliye karibu,”+ Yehova amesema, “nami nitamponya.”+
20 “Lakini waovu ni kama bahari inayorushwa-rushwa, wakati ambapo haiwezi kutulia, ambayo maji yake yanaendelea kurusha juu magugu-maji na matope. 21 Hakuna amani,” Mungu wangu amesema, “kwa waovu.”+