1 Wakorintho
Barua ya Kwanza kwa Wakorintho
1 Paulo, aliyeitwa kuwa mtume+ wa Yesu Kristo kupitia mapenzi ya Mungu,+ na Sosthene+ ndugu yetu 2 kwa kutaniko la Mungu lililo katika Korintho,+ kwenu ninyi ambao mmetakaswa+ katika muungano na Kristo Yesu, mlioitwa kuwa watakatifu,+ pamoja na wote ambao kila mahali wanaliitia jina+ la Bwana wetu, Yesu Kristo, Bwana wao na wetu:+
3 Na muwe na fadhili zisizostahiliwa+ na amani+ kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo.+
4 Sikuzote ninamshukuru Mungu kwa ajili yenu kwa sababu ya fadhili zisizostahiliwa+ za Mungu mlizopewa katika Kristo Yesu;+ 5 kwamba katika kila jambo mmetajirishwa+ katika yeye, katika uwezo kamili wa kusema na katika ujuzi kamili,+ 6 kama vile ushahidi juu ya Kristo+ ulivyofanywa kuwa imara katikati yenu, 7 ili kwamba msipungukiwe katika zawadi+ yoyote hata kidogo, huku mkiungojea kwa hamu ufunuo+ wa Bwana wetu Yesu Kristo. 8 Yeye pia atawafanya ninyi imara+ mpaka mwisho, ili msiwe na shtaka+ lolote katika siku+ ya Bwana wetu Yesu Kristo.+ 9 Mungu ni mwaminifu,+ aliyewaita kuingia katika ushirika+ pamoja na Mwana wake Yesu Kristo Bwana wetu.
10 Sasa nawahimiza+ ninyi, akina ndugu, kupitia jina+ la Bwana wetu Yesu Kristo kwamba nyote mseme kwa upatano,+ na kwamba kusiwe na migawanyiko+ katikati yenu, bali kwamba muunganishwe vema katika akili ileile na katika njia ileile ya kufikiri.+ 11 Kwa maana, ndugu zangu, wale wa nyumba ya Kloe walinifunulia+ juu yenu kwamba kuna magombano kati yenu. 12 Ninalomaanisha ni hili, kwamba kila mmoja wenu anasema: “Mimi ni wa Paulo,” “Lakini mimi ni wa Apolo,”+ “Lakini mimi ni wa Kefa,” “Lakini mimi ni wa Kristo.” 13 Kristo amegawanyika.+ Je, Paulo alitundikwa mtini kwa ajili yenu? Au je, mlibatizwa+ katika jina la Paulo? 14 Mimi nashukuru kwa kuwa sikubatiza hata mmoja wenu isipokuwa Krispo+ na Gayo,+ 15 ili yeyote asiseme kwamba mlibatizwa katika jina langu. 16 Ndiyo, niliibatiza pia nyumba ya Stefana.+ Kuhusu wale wengine, sijui kama nilimbatiza mwingine yeyote. 17 Kwa maana Kristo alinituma,+ si kwenda kubatiza, bali kwenda kutangaza habari njema, si kwa maneno ya hekima,+ ili mti wa mateso wa Kristo usifanywe kutofaa kitu.
18 Kwa maana neno juu ya mti wa mateso ni upumbavu+ kwa wale wanaoangamia,+ lakini kwetu sisi tunaookolewa+ ni nguvu za Mungu.+ 19 Kwa maana imeandikwa: “Nitaiangamiza hekima ya watu wenye hekima,+ na akili ya watu wenye akili+ nitaitupa kando.”+ 20 Yuko wapi mtu mwenye hekima? Yuko wapi mwandishi?+ Yuko wapi mwenye kubishania+ maneno wa mfumo huu wa mambo?+ Je, Mungu hakuifanya hekima ya ulimwengu iwe upumbavu?+ 21 Maana, kwa kuwa katika hekima ya Mungu, ulimwengu kupitia hekima yake+ haukuja kumjua Mungu,+ Mungu aliona vema kupitia upumbavu+ wa linalohubiriwa awaokoe wale wanaoamini.
22 Kwa maana Wayahudi wanaomba ishara+ na Wagiriki wanatafuta hekima;+ 23 lakini sisi tunamhubiri Kristo aliyetundikwa mtini,+ kwa Wayahudi ni sababu ya kujikwaa+ lakini kwa mataifa ni upumbavu;+ 24 hata hivyo, kwa wale walioitwa, Wayahudi na Wagiriki, Kristo ni nguvu+ za Mungu na hekima+ ya Mungu. 25 Kwa sababu kitu kipumbavu cha Mungu ni chenye hekima zaidi kuliko wanadamu, na kitu dhaifu cha Mungu ni chenye nguvu zaidi kuliko wanadamu.+
26 Kwa maana mnaona mwito wake kwenu, akina ndugu, kwamba si wengi wenye hekima+ katika njia ya kimwili walioitwa,+ si wengi wenye nguvu,+ si wengi wa uzawa wa cheo; 27 bali Mungu alivichagua vitu vipumbavu vya ulimwengu,+ ili awaaibishe watu wenye hekima; na Mungu alivichagua vitu dhaifu vya ulimwengu, ili aviaibishe vitu vyenye nguvu;+ 28 na Mungu alivichagua vitu vinyonge vya ulimwengu na vitu vinavyodharauliwa, vitu ambavyo si kitu,+ ili kuvifanya viwe si kitu+ vitu ambavyo ni kitu 29 ili mwili wowote usijisifu+ machoni pa Mungu. 30 Lakini ni kwa sababu yake kwamba ninyi mko katika muungano na Kristo Yesu, ambaye kwetu amekuwa hekima+ kutoka kwa Mungu, pia uadilifu+ na utakaso+ na kuachiliwa huru kupitia fidia;+ 31 ili iwe kama ilivyoandikwa: “Yeye anayejisifu, na ajisifu katika Yehova.”+