Mathayo
24 Sasa Yesu akaondoka, akashika njia kutoka hekaluni, lakini wanafunzi wake wakamkaribia na kumwonyesha majengo ya hekalu.+ 2 Akajibu, akawaambia: “Je, hamvioni vitu vyote hivi? Kwa kweli ninawaambia ninyi, Hakuna jiwe litakaloachwa hapa juu ya jiwe nalo lisiangushwe chini.”+
3 Alipokuwa ameketi juu ya Mlima wa Mizeituni, wanafunzi wakamkaribia faraghani, wakisema: “Tuambie, Mambo haya yatakuwa wakati gani, na ni nini itakayokuwa ishara ya kuwapo+ kwako na ya umalizio wa mfumo wa mambo?”+
4 Naye Yesu akajibu, akawaambia: “Jihadharini mtu yeyote asiwapotoshe;+ 5 kwa maana wengi watakuja kwa msingi wa jina langu, wakisema, ‘Mimi ndiye Kristo,’ nao watawapotosha wengi.+ 6 Mtasikia juu ya vita na habari za vita; angalieni kwamba msiogope. Kwa maana mambo hayo lazima yatukie, lakini ule mwisho bado.+
7 “Kwa maana taifa litasimama kupigana na taifa+ na ufalme kupigana na ufalme,+ kutakuwa na upungufu wa chakula+ na matetemeko ya nchi+ mahali pamoja baada ya pengine. 8 Mambo yote hayo ni mwanzo wa maumivu ya taabu.
9 “Ndipo watu watakapowatia ninyi katika dhiki+ na kuwaua+ ninyi, nanyi mtachukiwa+ na mataifa yote kwa sababu ya jina langu.+ 10 Ndipo, pia, watu wengi watakwazika+ na kusalitiana na kuchukiana.+ 11 Na manabii wengi wa uwongo+ watatokea na kuwapotosha wengi;+ 12 na kwa sababu ya kuongezeka kwa uasi-sheria+ upendo wa walio wengi zaidi utapoa.+ 13 Lakini yule ambaye atavumilia+ mpaka mwisho ndiye atakayeokolewa.+ 14 Na hii habari njema+ ya ufalme+ itahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote;+ na ndipo ule mwisho+ utakapokuja.
15 “Kwa hiyo, mtakapoona lile chukizo+ linalosababisha ukiwa, kama vile lilivyosemwa kupitia nabii Danieli, likiwa limesimama katika mahali patakatifu,+ (msomaji na atumie utambuzi,) 16 ndipo wale walio katika Yudea waanze kukimbilia+ milimani. 17 Mtu aliye juu ya paa ya nyumba asishuke kuchukua mali kutoka katika nyumba yake; 18 na mtu aliye shambani asirudi nyumbani kuchukua vazi lake la nje. 19 Ole wao wanawake wenye mimba na wale wanaonyonyesha mtoto mchanga katika siku hizo!+ 20 Endeleeni kusali kwamba kukimbia kwenu kusiwe wakati wa majira ya baridi kali, wala siku ya sabato; 21 kwa maana ndipo kutakapokuwa na dhiki kuu+ ya namna ambayo haijapata kutukia tangu mwanzo wa ulimwengu mpaka sasa,+ hapana, wala haitatukia tena. 22 Kwa kweli, kama siku hizo hazingefupishwa, hakuna chochote chenye mwili ambacho kingeokolewa; lakini kwa sababu ya wale waliochaguliwa+ siku hizo zitafupishwa.+
23 “Ndipo mtu yeyote akiwaambia, ‘Tazameni! Kristo huyu hapa,’+ au, ‘Pale!’ msiamini.+ 24 Kwa maana Makristo wa uwongo+ na manabii wa uwongo+ watatokea na kutoa ishara+ kubwa na maajabu ili kuwapotosha, ikiwezekana, hata wale waliochaguliwa.+ 25 Tazameni! Nimewaonya kimbele.+ 26 Kwa hiyo, watu wakiwaambia ninyi, ‘Tazameni! Yuko nyikani,’ msiende; ‘Tazameni! Yumo katika vyumba vya ndani,’ msiamini.+ 27 Kwa maana kama vile umeme+ unavyotokea sehemu za mashariki na kuangaza mpaka sehemu za magharibi, ndivyo kuwapo kwa Mwana wa binadamu kutakavyokuwa.+ 28 Popote mzoga ulipo, hapo ndipo watakapokusanyika+ tai.+
29 “Mara baada ya ile dhiki ya siku hizo jua litatiwa giza,+ nao mwezi+ hautatoa nuru yake, nazo nyota zitaanguka kutoka mbinguni, nazo nguvu za mbingu zitatikiswa.+ 30 Ndipo ishara ya Mwana wa binadamu+ itakapoonekana mbinguni, ndipo makabila yote ya dunia yatakapojipiga-piga yenyewe kwa kuomboleza,+ nayo yatamwona Mwana wa binadamu akija juu ya mawingu ya mbinguni akiwa na nguvu na utukufu mwingi.+ 31 Naye atawatuma malaika zake pamoja na mvumo mkubwa wa tarumbeta,+ nao watawakusanya pamoja watu wake waliochaguliwa+ kutoka kwenye zile pepo nne,+ kutoka mwisho mmoja wa mbingu mpaka mwisho wake mwingine.
32 “Basi jifunzeni jambo hili kutokana na mtini kama mfano: Mara tu tawi lake changa linapokuwa jororo na kutoa majani, mnajua kwamba kiangazi kiko karibu.+ 33 Vivyo hivyo ninyi pia, mnapoona mambo yote hayo, jueni kwamba yuko karibu milangoni.+ 34 Kwa kweli ninawaambia ninyi kwamba kizazi hiki+ hakitapitilia mbali kamwe mpaka mambo yote hayo yatukie. 35 Mbingu na dunia zitapitilia mbali,+ lakini maneno yangu hayatapitilia mbali kamwe.+
36 “Kuhusu siku ile na saa+ ile hakuna mtu anayejua, wala malaika wa mbinguni wala Mwana, ila Baba tu.+ 37 Kwa maana kama vile siku za Noa+ zilivyokuwa, ndivyo kuwapo kwa Mwana wa binadamu kutakavyokuwa.+ 38 Kwa maana kama vile walivyokuwa katika siku hizo kabla ya gharika, wakila na kunywa, wanaume wakioa na wanawake wakiolewa, mpaka siku ambayo Noa+ aliingia ndani ya safina;+ 39 nao hawakujali mpaka gharika ikaja na kuwafagilia mbali wote,+ ndivyo kuwapo kwa Mwana wa binadamu kutakavyokuwa. 40 Wakati huo watu wawili watakuwa shambani: mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa; 41 wanawake wawili watakuwa wakisaga kwenye jiwe la kusagia:+ mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa.+ 42 Kwa hiyo, endeleeni kukesha kwa sababu hamjui ni siku gani Bwana yenu atakuja.+
43 “Lakini jueni jambo moja, kwamba ikiwa mwenye nyumba angalijua mwizi anakuja katika kesha gani,+ angaliendelea kukaa macho na hangaliruhusu nyumba yake ivunjwe. 44 Kwa hiyo ninyi pia iweni tayari,+ kwa sababu Mwana wa binadamu atakuja katika saa msiyofikiria.
45 “Ni nani kwa kweli mtumwa mwaminifu na mwenye busara+ ambaye bwana wake alimweka rasmi juu ya watumishi wake wa nyumbani, awape chakula chao kwa wakati unaofaa?+ 46 Mtumwa huyo atakuwa mwenye furaha+ ikiwa bwana wake atakapofika atamkuta akifanya hivyo! 47 Kwa kweli ninawaambia ninyi, Atamweka juu ya mali zake zote.+
48 “Lakini mtumwa huyo mwovu akisema moyoni mwake,+ ‘Bwana wangu anakawia,’+ 49 naye aanze kuwapiga watumwa wenzake na kula na kunywa pamoja na walevi wa kupindukia, 50 bwana wa mtumwa huyo atakuja katika siku ambayo hatazamii na katika saa+ ambayo hajui, 51 naye atamwadhibu kwa ukali+ mkubwa zaidi na kumgawia sehemu yake pamoja na wanafiki. Huko ndiko atalia na kusaga meno.+